Quantcast
Channel: SUFIANIMAFOTO
Viewing all articles
Browse latest Browse all 13053

*NIMEACHA UNGA, BANGI MASHABIKI WATAKOMAJE? SUPER STAR BAND IMENIBADILISHA-MSAFIRI DIOUF

$
0
0
''Nimeacha Unga na Bangi, sasa mashabiki watakoma na mavitu yangu, Bendi ya Super Star imenibadilisha, hivi sasa mimi ni mwingine kabisa na mwili wangu si unauona???, nanenepa sasa''. alisema Diouf. CHEKI VIDEO YA WIMBO WA AFRICAN UNITY HAPA CHINI
MWANAMUZIKI na Rapa mahiri wa muziki wa dansi nchini, alitua nchini akitokea nchini kenya kupiga kazi miaka ya 2003 na kujiunga na bendi ya Twanga Pepeta baada ya kufanya kazi nzuri katika albam ya Special Remix ya Ally Choki na Gurumo, Msafiri Diouf, amesema kuwa hivi sasa ameamua kuacha kula unga na kuvuta bangi.

Akizungumza na mtandao huu wa www.sufianimafoto.com, Diouf, alisema kuwa ameamua kuachana na madawa hayo baada ya kuona kuwa anaendelea kuyumba katika kazi zake za kimuziki na kuona anazidi kupotea na zaidi kupoteza mashabiki wake waliomkubari tangu alipotua nchin na kuonyesha uwezo wa kurap, kuimba na kutunga miaka ya 2003.    Diouf alipoyua nchni akitokea Jiji la Nairobi alikokuwa akifanyia kazi, alifikia nyumbani kwa aliyekuwa mpiga gita la besi wa bendi ya Tam Tam, marehemu  Msichoke Kombo, ambaye alimuunganisha na kupata kazi katika bendi hiyo.     Aidha Diouf baada ya kupata kazi katika bendi hiyo iliyokuwa chini ya Kocha wa Dunia Muumin Mwinjuma, hakuweza kudumu nayo kwa muda mrefu ambapo alikaa kwa muda wa miezi mitatu tu na kupata shavu la kufanya kazi na Ally Choki katika Albam yake ya Special Remix na kufanya vizuri zaidi katika wimbo wa marudio wa Gurumo wa Usia wa Baba, ambapo alionyesha uwezo mkubwa na baada ya hapo alijiunga rasmi na bendi ya Twanga Pepeta akipelekwa na Ally Choki aliyekuwa akitambua vilivyo uwezo wake toka walipokuwa pamoja huko Jijini Nairobi.  

Alipotua Twanga pia alionyesha uwezo mkubwa wa kuimba na kurap na kuibuka na baadhi ya nyimbo zilizopata umaarufu na kufanya vizuri katika vituo mbali mbali vya redio na Televisheni kama wimbo wa Afrcan Unity, Safari 2005 uliobeba jina la Albam na Shafii uliokuwa katika albam ya Mtu Pesa.

 Kadri siku zilivyozidi kwenda Rapa huyo mahiri alizidi kupotea kwa kuanza kutumia madawa, jambo ambalo lilianza kumpotezea umaarufu kwa kudharaulika huku akianza kushindwa kufanya kazi vizuri jukwaani ikiwa ni pamoja na kukata sauti, kushindwa kuimba kwa kiwango kilichozoeleka, kutokaa jukwaani kwa muda mwingi na hata kuchelewa kazini ama kutokuwepo wakati wimbo anaotakiwa kuimba unapopigwa na kuimbwa na mwanamuziki mwingine. 

Diouf, alikili kuwa ni kweli akikuwa ameshapotea katika Anga za Muziki, na kusema kuwa anaishukuru sana bendi ya Super Star na uongozi wake kwa kumbadilisha na kujikuta akimudu kuacha kuendelea na kutumia madawa hayo na badala yake akibadilika na kupiga kazi zaidi.

Bendi ya Super Star, imeundwa na baadhi ya wanamuziki aliokuwa nao katika bendi ya Twanga Pepeta, kama mpiga Kinanda, Victor Mkambi, mwimbaji Amigolasi, mwimbaji mwingine aliyekuwa na bendi ya Extra Bongo, Rogat Hegga 'Katapila' na wengineo.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 13053

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>