Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikata utepe huku akishirikiana na viongozi mbalimbali ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa mtambo wa wa 10,000 wa Biogas hapa nchini. Mtambo huo unaomilikiwa na Ndugu Bakari Seif na Mkewe Mwanaidi Said (wa pili na wa tatu kutoka kushoto). Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Ndugu Eliakim Maswi, kulia kwa Mama Salma ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Ndugu Mwantumu Mahizana. Aliyesimama kushoto ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Kondo Ndugu Ramadhan Seleman akifuatiwa na Mkurugenzi Mkuu wa CARMATEC Ndugu Elifariji Makomgoro.
↧