Malori yaliyogongana yakiwa yameziba njia baada ya kugongana eneo la mto wami
Foleni ni kubwa sana ya mabasi yaendayo mikoa ya Tanga,Arusha Na Kilimanjaro.
Ajali mbaya imetokea eneo la mto wami na kusababisha foleni kubwa kwa mabasi na magari yanayotumia njia hiyo, Chanzo cha ajali hiyo inadaiwa ni kufeli breki kwa malori hayo yakiwa yanateremka kwenye mlima huo.
Polisi wanaendelea na jitihada za kuyatoa ili njia ipatikane kwa ukubwa zaidi ili kuruhusu upitaji mzuri wa magari.Picha na Dj Seki