Quantcast
Channel: SUFIANIMAFOTO
Viewing all articles
Browse latest Browse all 13053

*UZINDUZI RASMI WA MAISHA PLUS/ MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2013 , KINGOLWIRA MOROGORO

$
0
0
Masoud Kipanya, Mkurugenzi Mtendaji wa Maisha Plus, akizungumza na wananchi waliofika kushuhudia uzinduzi wa Maisha Plus/Mama Shujaa wa Chakula 2013 Kingolwira Morogoro , pia kumkaribisha Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Anthony Mtaka kufanya uzinduzi huo.
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Anthony Mtaka, Akizungumza na wakazi wa eneo la Kingolwira pamoja na wageni na kutoa tamko rasmi la  kuzindua  shindano la Maisha Plus/ Mama shujaa wa chakula 2013.
Mama Shujaa wa Chakula 2012 Sister Matha Mwasu aliyeshika nafasi ya kwanza , Akizungumza katika uzinduzi huo. 
 Mshindi wa Shindano la Maisha Plus, Bernick Kimiro, akizungumza na wageni waalikwa pamoja na wenyeji wa eneo la Kingolwira Morogoro, kwa kuwasisitiza vijana wajitokeze kuchukua fomu za ushiriki katika shindano la Maisha Plus/ Mama Shujaa wa Chakula 2013 ambazo sasa zimeanza kutolewa na kuwaeleza kuwa shindano hilo linatoa Fursa nyingi za kimaendeleo na kilimo kwa ujumla.
 Bwana Bonda ambaye ni mmoja wa wakurugenzi Maisha Plus.
Mdau kutoka OXFAM Bill Marwa Akiwa anafuatilia kwa umakini uzinduzi wa Maisha Plus/ Mama Shujaa wa Chakula 2013
Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa Maisha Plus/ Mama shujaa wa Chakula 2013 Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Anthony Mtaka  akifanya uzinduzi wa aina yake wa Maisha Plus/ Mama Shujaa wa Chakula 2012/13 kwa kufukua fomu ambazo zilikuwa zimefukiwa ikiwa ni kielelezo cha kilimo kwanza.
Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Anthony Mtaka akimkabidhi Fomu ya kwanza ya ushiriki kwa Bi. Nuru Saidi Mbonga kutoka Dakawa ikiwa ni fomu ya Mama shujaa wa Chakula 2013
Mheshimiwa   Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Anthony Mtaka Akimkabidhi fomu ya Ushiriki wa Maisha plus kwa vijana Bi. Shamimu Ramadhani
 Mmoja ya Vijana wakiume nae akiwa anakabidhiwa fomu ya ushiriki na Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Anthony Mtaka
Wakiwa wanasoma fomu na kujiandaa kuzijaza 
Waliovaa T-Shirt za Rangi nyeusi ni Wadau wa OXFAM.
 Burudani za Ngoma zikiendelea
 Burudani za aina yake zikiendelea
 Wazee kutoka eneo la Kingolwira wakiwa wamekuja kushuhudia uzinduzi huo
 Wadau kutoka Sehemu mbalimbali wakiwa wamekuja shuhudia uzinduzi huo
 Mkurugenzi Mtendaji wa Maisha Plus Ali Masoud 'Kipanya' akifunga sherehe fupi za uzinduzi wa Maisha Plus 2013.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 13053

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>