JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAWIZARA YA UCHUKUZIMAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Simu: 255 22 2460735/2460706-8Faksi: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056Barua pepe: met@meteo.go.tz
DAR ES SALAAM
Tovuti: www.meteo.go.tz
Kumb.No. TMA/1622 01 April, 2014
TAARIFA KWA UMMAMwelekeo wa Kimbunga
“
H
ELLEN”
na hali ya Mvua
Mamlaka ya Hali ya Hewa imeendelea kufuatilia kwa karibu mifumo ya hali ya hewa namabadiliko yake pamoja na adhari zake kwa Nchi yetu na kutoa utabiri na tahadhari za halimbaya ya hewa. Tarahe 28 Machi 2014 mgandamizo mdogo wa hewa katika eneo la Rasi yaMsumbiji kusini magharibi mwa bahari ya Hindi ulianza kuimarika zaidi na kusababishakuwepo kwa makutano ya upepo na mwelekeo wa vipindi vya mvua kubwa katika maeneomengi nchini. Tarehe 29 Machi 2014 mgandamizo huo wa hewa (Tropical Depression)
uliimarika zaidi na kuwa kimbunga kilichopewa jina ‘
Hellen’
(Tropical Cyclone) uchambuziulionesha kuwa kimbunga
‘Hellen’
kilitarajiwa kuongezeka nguvu (Severe Tropical Cyclone)na kusababisha aongezeko zaidi la mvua na upepo mkali. Hivyo maeneo yafuatayo yalitabiriwakuwa na adhari zaidi za mabadiliko hayo kuanzia tarehe 30 Machi hadi 01 April 2014 ; Mikoaya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam, Tanga, visiwa vya Unguja na Pemba, pamoja na mikoaya Dodoma, Singida, Ruvuma, Katavi, Njombe, Iringa, Mbeya na Morogoro.
Viwango vya mvua zaidi ya mm 50 kwa saa 24 zilizopimwa tarehe 30 Machi hadi Asubuhiya tarehe 01 Aprili 2014.
Tarehe 30Machi- 01April 2014Morogoro 71.9mm, Mahenge 70.2mm na Ilonga 64.7mm.
Mwenendo wa Kimbunga Hellen katika kipindi cha saa 24 Zilizopita
.
Katika kipindi hicho nguvu ya Kimbunga ‘
Hellen’
ilibadilika mara kwa mara na katika vipindivifupi hususan kilipokaribia pwani ya kaskazini magharibi mwa kisiwa cha Madagasca, hivyokubadili pia mifumo ya hali ya hewa na viwango vya mvua vilivyotarajiwa katika baadhi yamaeneo ambayo tahadhari ilitolewa
. Hata hivyo kimbunga ‘
Hellen’
bado kipo katika eneo la rasiya Msumbiji karibu na pwani ya Kisiwa cha Madagascar ambapo kitaendelea kusababisha

mabadiliko ya mvua katika maeneo machache, hususan katika Mikoa ya Mtwara, Lindi,Ruvuma, Njombe, Mbeya na Rukwa.Mvua za Masika zinatarajiwa kuendelea katika maeneo mbalimbali nchini kama zilivyotabiriwa.Mamlaka inaendelea kufuatilia mifumo ya hali ya hewa na kutoa taarifa na tahadhari kilainapobidi.Imetolewa na
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzani